Kiongozi wa Democrat Ataka Trump Aondolewe Baada ya Ripoti ya Mueller

Siku moja baada ya kuchapishwa kwa ripoti ya mchunguzi maalum Robert Mueller juu ya ushawishi wa Urusi kwenye uchaguzi wa Marekani, viongozi kadhaa wa ngazi za juu kwenye chama cha Democrat wameanza kutoa wito wa kuondolewa madarakani kwa Rais Donald Trump.

Elizabeth Warren, aliyetangaza nia ya kuwania urais kupitia chama hicho, ameandika kwenye mtandao wa Twitter kwamba ripoti ya Mueller imeonesha ukweli kwamba "serikali hasimu ya kigeni iliushambulia uchaguzi wa 2016 kumsaidia Trump na mwenyewe Trump aliupokea msaada huo, na baada ya kuchaguliwa akataka kuzuwia uchunguzi dhidi ya mashambulizi hayo.

" Warren amesema sasa ni jukumu la Baraza la Congress kuchukuwa hatua za kukataa matumizi mabaya ya madaraka ili kulinda heshima ya utawala wa sheria.

 Hata hivyo, spika wa Baraza la Wawakilishi kutokea chama cha Democrat, Nancy Pelosy, amesema hatopigania kura ya kumuondoa madarakani, ikiwa hakupata hakikisho la uungwaji mkono wa wajumbe wa Republican.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad