Kiongozi wa Kundi la Islamic State ajitokeza baada ya miaka 5

Kiongozi wa kundi la Islamic State,  Abu Bakr al-Baghdadi ameonekana katika kanda ya video, hata hivyo haijulikani ni lini kanda hiyo ya video ilirekodiwa. Kiongozi huyo hajaonekana tangu 2014, wakati alipodai kuunda taifa linalofuata sheria ya kiislamu nchini Syria na Iraq.

Katika kanda yake mpya, Baghdad alikiri kupoteza eneo la Baghuz ambalo ndio ngome ya mwisho ya kundi hilo katika eneo hilo. IS inasema kuwa ilichukuliwa mnamo mwezi Aprili, kanda hiyo ya video ilichapishwa katika tovuti ya kundi hilo ya al-Furqan.

Msemaji wa wizara ya kigeni nchini Marekani anasema kuwa kanda hiyo itachunguzwa ili kubaini inakotoka, huku ikiongezea kwamba muungano wa majeshi ya Marekani utaendelea kuhakikisha kuwa kiongozi yeyote wa kundi hilo aliyesalia anakamatwa mara moja.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad