Mkuu wa UN Ataka Mashambulizi Kusitishwa Libya

Mkuu wa UN Ataka Mashambulizi Kusitishwa Libya
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali kuongezeka kwa makabiliano ya kijeshi karibu na mji wa Tripoli na kutoa wito wa kusitishwa mapigano maramoja nchini Libya.

Ombi lake limefuatia shambulizi la angani lililofanywa na vikosi vya kamanda Khalifa Haftar kwenye Uwanja wa ndege wa Mitiga mashariki mwa Mji Mkuu wa Tripoli.

Taarifa ya Umoja wa Mataifa imesema kuwa Guterres amezitaka pande hizo mbili zinazohasimiana zisitishe mapigano ili kuepusha kuzuka kwa mzozo mkubwa nchini humo, Shambulizi hilo la angani lilisababisha kufungwa kwa Uwanja huo pekee wa ndege ambao unafanya kazi mjini Tripoli wakati makabiliano yakipamba moto karibu na mji huo mkuu na maelfu ya watu kukimbia.

Haftar alianzisha wiki iliyopita operesheni ya kukamata Tripoli wakati Guterres alikuwa nchini Libya kushinikiza makubaliano ya kisiasa kuhusu kuandaliwa uchaguzi.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad