Mtuhumiwa wa mashambulio ya misikiti Christchurch kupimwa afya ya akili

Mtuhumiwa wa mashambulio ya misikiti Christchurch kupimwa afya ya akili
Mtuhumiwa wa mauaji ya watu 50 kwenye mashambulizi ya misikiti miwili mwezi uliopita nchini New Zealand ameamriwa kupimwa akili.

Kwa mujimu wa Jaji wa Mahakama Kuu, Cameron Mander, mtuhumiwa huyo atapimwa na madaktari bingwa wa afya ya akili ili kuamua iwapo anaweza kuendelea na kesi hiyo ama ni mgonjwa wa akili.

Mtuhumiwa huyo anakabiliwa na mashtaka 50 ya mauaji na mashtaka 39 ya kujaribu kuua.

Raia wa Australia Brenton Tarrant, 28, alihudhuria kesi hiyo kwa njia ya simu ya mtandao kutokea gerezani. Chumba cha mahakama kilijaa ndugu za watu ambao waliuawa kwenye mashambulizi hayo.


Mashambulio hayo ni makubwa zaidi katika historia ya taifa la New Zealand.


Waziri Mkuu wa nchi hiyo aliiita siku ya mashambulizi kuwa ni moja ya siku za kiza zaidi kwa New Zealand.

Pia ameazimia kupiga marufuku umiliki kwa raia wa silaha zote za sampuli ya kivita.

Nini kilitokea mahakamani?
Jaji Mander ameamuru mtuhumiwa achunguzwa afya yake ya akili mara mbili ili ibainike yupo katika hali gani.

Mtuhumiwa huyo alikuwa kimya akisikiliza kwa makini kilichokuwa kikiendelea mahakamani. Hakuongea kitu.

Aliweza kuwaona jaji na wanasheria tu, kamera haikuelekezwa walipo wasikilizaji wa kesi.

Jaji ameamuru aendelee kusalia rumande mpaka pale kesi yake itakapotajwa tena Juni 14.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad