Ommy Dimpoz Arejea Ujerumani Kwaajili ya Kufanyiwa Uchunguzi



Msanii wa Bongofleva Ommy Dimpoz, amethibitisha kurejea hospitalini huko Ujerumani kwaajili ya kufanyiwa uchunguzi wa afya yake.

Dimpoz amerudi Ujerumnai ikiwa ni miezi kadhaa imepita tangu afanyiwe upasuaji wa koo mwaka jana.


Hata hivyo kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ommy ameweka wazi kuwa uchunguzi huo umekwenda salama na amemshukuru Mungu kwa hilo. ''Alhamdulilaah Mungu Ni Mwema'' #CheckupsDone.

Ommy alikaa nje ya muziki kwa muda, kufuatia kusumbuliwa na tatizo la koo ambapo alianza kwa kupata matibabu nchini Kenya kisha Afrika Kusini na baadaye Ujerumani.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad