R Kelly Ashindwa kufika Mahakamani, Aliye Mfungulia Mashtaka Ashinda Kesi

R Kelly Ashindwa kufika Mahakamani, Aliye Mfungulia Mashtaka Ashinda Kesi
Mwanamke mmoja aliyefungua kesi ya unyanyasaji wa kingono dhidi ya RKelly ameshinda kesi baada ya nguli huyo wa R&B kushindwa kufika mahakamani.
.
Mwanamke huyo ambaye anadai kuwa Kelly alikuwa akimfanyia vitendo vya unyanyasaji wakati ana umri wa miaka 16 alifungua mashtaka siku moja kabla #RKelly hajakamatwa kwa kesi za unyanyasaji wa kingono mwezi februari.
.
Kesi itasikilizwa tena mwezi ujao ambapo jaji ataamua kiasi ambacho @Rkelly atatakiwa kulipa. Rkelly hata hivyo hajawahi kukubali shtaka lolote la unyanyasaji wa kingono japo hata sasa anakabiliwa na kesi nyingine 10 tofauti za masuala hayo hayo ya unyanyasaji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad