Tiwa Savege na Victoria Kimani Katika Vita Nzito Mtandaoni....

Tangu Mwanamuziki wa Nigeria @iamkizzdaniel ameachia ngoma yake mpya “Fvck You” Mastaa mbalimbali Afrika wamemuumga mkono kwa kuirudia kwenye challenge maarufu kwasasa #FvckYouChallenge, Staa wa muziki wa Kenya @victoriakimani ni mmoja ya wasanii waliourudia wimbo huo lakini lakini wake umeleta utata.
.
Kwenye cover yake, Kimani anasikika akimchana vibaya mno @iam_ycee kuhusu tabia yake ya wizi wa mistari na pia anarusha madongo mazito ambayo yanadaiwa kumlenga @Tiwasavage, anasema “Umeshakuwa mzee wa miaka 45 alafu bado unajiuza na kujiita African Bad gyal”

@iamseyishay ambaye pia amefanya challenge hiyo na kudaiwa pia kumkandia Tiwa Savage alicomment kwenye Post ya Victoria Kimani, comment ambayo ilichochea kuwa wote pamoja wanampiga madongo Tiwa Savage.

Siku ya jana #TiwaSavage alijibu mashambulizi kwa kuweka picha ya ndinga yake mpya na kuipa caption ya “Na anaendelea kunibariki” baada ya muda #VictoriaKimani alimjibu tena (Ameishaifuta hiyo Post) kwa kumkandia tena kuwa anajua amepata pesa za kununulia gari hilo kwa wanaume wa watu.

Chanzo cha bifu linalochipukia kati ya mastaa hao wawili wa kike Afrika bado hakijajulikana.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad