Hizi Hapa Kauli za Jakaya Kikwete na Kamanda Sirro Juu ya Utata wa Kifo cha Reginald Mengi


Pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia msiba wa mzee wetu. Mungu aendelee kumpumzisha kwa amani Dkt. Reginald Mengi. Amen!

Tangu zitangazwe taarifa za ghafla za kifo chake, kumetokea taarifa tata zinazodai kifo chake kina mkono wa mtu. Taarifa hizi zinaongozwa na mwanaharakati Mange Kimambi ambaye amefika mbali zaidi kwa kumtaja mke wa marehemu, Jacky na kijana Hussein wa Element kuhusika.

Awali zilionekana kama taarifa za umbea tu na uzushi lakini kwa kadri zinavyoanza kuzungumzwa na watu nyeti, jumlisha na kucheleweshwa kwa mwili wa marehemu, lipo jambo!

IGP Sirro amesema mwili ukishazikwa, Jeshi la Polisi litaanza kufuatilia ukweli wa kinachozungumzwa mitandaoni.

Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete nae amesema tusubiri ndugu wa marehemu waliopo Dubai waje wafafanue. Kwamba, ukweli utajulikana wakishawasili nchini. 

Hizi sio kauli nyepesi. Kama wao hawakupuuza, basi kuna mtiti unaendelea huko ambao unaonekana kufichwa fichwa!

Huenda wengi wetu tulishaamua kupuuza vijimaneno vilivyojitokeza na kumuombea mzee apumzike kwa amani, lakini hizi kauli zilizotolewa leo na zinazoendelea kutolewa zinatengeneza shauku ya kujua kuna nini cha ziada?

Source:Interest/JF
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad