IGP Sirro: Tutafuatilia Yote Yanayosemwa Mitandaoni Kuhusu Reginald Mengi...Kwa Sasa Tumalize kwanza Msiba

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro amesema  Jeshi lake litafuatilia kwa kina maneno yote yanayosemwa  mitandaoni kuhusu Kifo cha Reginald Mengi ili kubaini kama yanaukweli wowote ili sheria ichukue mkondo wake.

IGP Siiro ametoa kauli hiyo leo baada ya kufika nyumbani kwa Dr Mengi ili kutoa Pole ya msiba.

”Mzee Mengi alikuwa mshauri mzuri sana kwenye masuala ya ulinzi na usalama pamoja na misaada midogo midogo kwa vijana wetu wanapokuwa na shida. Zaidi alikuwa ‘very humble’ mara zote alikuwa anajishusha sana.

"Yako mengi yanayoongelewa kwa sasa mitandaoni, lakini jambo la msingi tumalize kwanza msiba, hayo yanayozungumzwa mitandaoni tutafuatilia,” amesema Sirro.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad