Miili ya wavuvi waliokatwa Mapanga na Boko Haram yapatikana


Takriban miili kumi ya wavuvi ambao inadaiwa walikatwa panga hadi kufa na kikundi cha kigaidi cha Boko Haram ilipatikana jana karibu na mji wa Maiduguri kaskazini mashariki mwa Nigeria, Afisa wa usimamizi wa dharura wa eneo hilo alisema.

Kundi hilo la wavuvi walishambuliwa siku ya Alhamisi huko Alou Dam,kilomita 4 kutoka Maiduguri,mji mkuu wa kaskazini mwa Borno.

Bello Danbatta, mkuu wa Shirika la Usimamizi wa Dharura la Borno, alisema kuwa wengi wavuvi walikuwa wametoka kijiji jirani cha Konduga.

Kundi hilo la kigaidi la Boko Haram limesababisha vifo vya takriban watu 20,000 tangu mwaka wa 2009 na kuwaacha watu zaidi ya milioni 2.6 bila makazi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad