Msemaji wa Serikali Azungumzia Kifo cha Dkt. Reginald Mengi


Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas ameeleza kuguswa na kifo cha Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Dkt. Reginald Mengi.

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mwenyekiti wa IPP, Mzee Reginald Mengi. Kama alivyopata kusema yeye mwenyewe siku za uhai wake kuwa watu wanaoacha alama hawafi, basi mawazo, falsafa, ubunifu na kujitoa kwake vitaendelea kuishi nasi," ameeeleza Dkt. Abass.

Taarifa rasmi zinaonyesha kuwa Mzee Reginald Abraham Mengi amefariki dunia akiwa huko Dubai (UAE). Mzee Mengi alizaliwa mwaka 1944 mkoani Kilimanjaro.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad