Sudan: Vyama vya upinza na Chama tawala vyakubaliana

Chama tawala na vyama vya upinzani nchini Sudan, vimekubaliana kujipa muda wa miezi sita ili viweze kuunda serikali ya pamoja.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na jumuiya ya ushirikiano wa maendeleo ya nchi za Afrika Mashariki na pembe ya Afrika IGAD makubaliano hayo yaliyofanyika siku ya Ijumaa ni sehemu ya mazungumzo ya amani yaliyotiwa sahihi mwezi Septemba mwaka jana.

Jumuiya hiyo ambayo imekuwa ikisaidia kusimamia mazungumzo ya amani kati ya pande hizo mbili imesema makubaliano mapya yatawasilishwa kwenye baraza la mawaziri huko Juba wiki ijayo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad