Tanzania Yaporomoka Katika Orodha ya Uhuru wa Vyombo vya Habari

Ikiwa leo ni siku ya Uhuru wa Habari duniani, Tanzania imeporomoka kwa nafasi 25 katika viwango vya Uhuru wa Habari Duniani hadi nafasi ya 118 kwa mwaka 2019 kutoka nafasi ya 93 mwaka 2018 kati ya nchi 180


Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Waandishi wa Habari Wasio na Mipaka (Reportes Without Borders), sekta ya habari nchini Tanzania imekumbana na changamoto mbalimbali kufuatia kupitishwa kwa sheria inayoonekana kuwa kandamizi, kufungwa kwa vyombo vya habari, na kufukuzwa kwa wanahabari nchini


Kwa mujibu wa ripoti hiyo mambo mengine yaliyochangia Tanzania kuporomoka kwa kiwango hicho ni tukio la kuvamiwa kwa Clouds Media Group mwaka 2017, kufungiwa kwa baadhi ya vyombo vya habari na waendeshaji wote wa tovuti na blogu za habari kutakiwa kujisajili na kulipa ada ili kuweza kutoa huduma hiyo


Matukio yaliyotikisa sekta ya habari ni kukamatwa watumishi wawili wa Tume ya Kulinda Waandishi wa Habari (CPJ), Novemba 2018 ambao walikuja nchini kufahamu changamoto zinazowakumba waandishi wa habari


Aidha, tukio jingine ni kupotea katika mazingira ya kutatanisha kwa mwandishi wa kujitegemea, Azory Gwanda aliyekuwa akichunguza mauaji ya viongozi wa Serikali za mitaa mkoani Pwani  - #regrann  

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad