Trump Amshambulia Robert Mueller, Asema Anawindwa Kama Mchawi

Trump Amshambulia Robert Mueller, Asema Anawindwa Kama Mchawi
Rais Donald Trump wa Marekani amedai ananyanyaswa, na amemshambulia mwanasheria maalum Robert Mueller aliyeongoza jopo lililochunguza kuingilia kwa Urusi katika uchaguzi wa mwaka 2016 nchini Marekani.

Haya yanajiri siku moja baada ya Mueller kufafanua sababu iliyomzuia kumfungulia Rais Trump mashitaka ya kujaribu kuzuia mchakato wa kimahakama. Kupitia ukurasa wake maarufu wa mtandao wa twitter, Trump ameandika leo kwamba anafanyiwa unyanyasaji ambao haujawahi kumkabili rais mwingine katika historia ya Marekani.

Vile vile ameukosoa uchunguzi ulioongozwa na Robert Mueller, akiuita 'windo la kumsaka mchawi' ambalo limegharibu dola milioni 40. Akizungumza hapo jana kwa mara ya kwanza tangu kuchapishwa kwa ripoti ya uchunguzi wake, Mueller alisema kumfungulia mashtaka Trump haikuwa mojawapo ya malengo ya uchunguzi, kwa sababu kanuni za wizara ya sheria ya Marekani haziruhusu uchunguzi dhidi ya rais aliyeko madarakani.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad