Wakurugenzi hawana mamlaka na fedha za mfuko wa jimbo

Wakurugenzi wa halmashauri nchini hawaruhusiwi kutumia fedha za mfuko wa jimbo bila idhini ya mwenyekiti wa mfuko huo ambaye ni mbunge.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Jumatatu Mei 13, na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mwita Waitara wakati akijibu swali la Mbunge wa Konde, Khatibu Said Haji (CUF).

Katika swali lake, mbunge huyo alitaka kujua kuhusu umuhimu wa Serikali kuongeza viwango vya fedha ili kuleta ufanisi.

Aidha, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye ulemavu, Jenista Mhagama, amesema serikali itatoa waraka mpya kuhusiana na fedha hizo kuwakumbusha wakurugenzi kwamba hawana mamlaka na fedha hizo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad