Watu 7 Wafariki Wengine 12 Wajeruhiwa Baada ya gari Aina ya Noah Kupata Ajali Kigoma

Watu 7 wamefariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupasuka tairi la nyuma na kupinduka mkoani Kigoma.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Martin Ottieno amesema ajali hiyo ilitokea jana saa 12 :15 jioni katika kijiji cha Mlela wilayani Uvinza mkoani humo.



Alisema gari hiyo iliyokuwa inatokea wilayani Uvinza kwenda Kigoma mjini ilipasuka tairi la nyuma upande wa kushoto na kupinduka. Majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Mkoa ya Maweni.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad