Hii ndio sababu ya Nicki Minaj kutokuwepo kwenye ziara ya Chris Brown




Baada ya kusambaa kwa taarifa za rapper Nicki Minaj kutokuwepo kwenye list ya majina ya wasanii watakaotumbuiza na mkali wa RnB Chris Brown kwenye ziara yake ya muziki “IndiGOAT” inayotangazwa kuanza hivi karibuni.

Sasa mtandao wa TMZ umeripoti kuwa Nicki Minaj hakuwahi kusaini mkataba wa kufanya ziara na Chris Brown na kuelezwa kuwa ndio maana hajatokea kwenye list hiyo japo waliwahi kujadili kufanya kitu kama hicho baada ya wimbo wao wa ‘Wobble Up’ kufanya vizuri na kufikisha watazamaji Mil.22 tokea uachiwe kwenye mtandao wa YouTube May 20,2019.

Chris Brown alitaja list ya wasanii watakaomsindikiza kwenye ziara yake kupitia ukurasa wake wa Twitter huku list hiyo inawakutanisha wakali kama Torylanes, Tydollasign, JoynerLucas na Yella Beezy.
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. KWANI PICHA NA MAELEZO YA HABARI YANAOANA ??????

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad