Lazaro Nyalandu: CHADEMA Itashinda Majimbo Yote Singida Uchaguzi Mkuu wa Mwakani

Kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Lazaro Nyalandu, amedai kuwa mwaka 2020, chama hicho kitarejesha majimbo yote ya Mkoa wa Singida ikiwamo jimbo alilokuwa akiliongoza la Singida Kaskazini.

Akizungumza katika Kijiji cha Ikungi mkoani Singida  wiki iliyopita, kada huyo alisema kutokana na kazi ya kujenga chama katika mkakati maalum unaofahamika katika chama hicho kama ‘Chadema ni msingi, chama hicho kitaibuka na ushindi katika majimbo yote ya mkoa wa Singida.

“Kama vile huu mkoa wa Singida ulivyokuwa na watu wawili maarufu yupo Tundu Lissu na yupo Nyalandu, sasa timu hii inacheza pamoja ,tutaichukua Singida Mashariki tena, tutaichukua Singida Kaskazini kwa mara ya kwanza ,tutashinda Singida Magharibi, majimbo yote mawili ya Iramba na Itigi”, Nyalandu alisema.

Kada huyo wa Chadema ambaye pia aliwahi kuwa mbunge wa Singida Kaskazini na Waziri wa Maliasili na Utalii katika Serikali ya awamu ya nne, hivi karibuni alikamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na wenzake wawili akituhumiwa kwa rushwa na mikutano iliyokatazwa na Serikali.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad