Watoto 500 Wenye Matatizo ya MOYO Wakwama Muhimbili, PAUL Makonda Atoa Milioni 120 Upasuaji wa Watoto 60

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda leo Juni 22 ametimiza ahadi ya kutoa ufadhili wa matibabu ya upasuaji wa moyo kwa watoto 10 kati ya 60 alioahidi kugharamia matibabu yao hadi pale watakapopona.

RC Makonda amesema ameamua kutoa ufadhili wa watoto 10 kila mwezi kwa kipindi cha miezi sita ambapo zoezi la upasuaji kwa watoto hao litaanza rasmi siku ya Jumatatu ya Juni 24, 2019 kwenye Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete.

Akizungumza wakati wa hafla ya kupokea hundi ya Shilingi Milioni 10 kutoka taasisi ya Patel Samaj kwaajili ya matibabu ya watoto 10 kati ya 60 kutoka mikoa mbalimbali RC Makonda amesema walengwa ni watoto wanaotoka kwenye familia maskini ambazo zimepoteza matumaini kutokana na ukubwa wa garama za matibabu ambapo inaelezwa gharama ya upasuaji ni kwa mtoto mmoja ni kati ya Shilingi Milioni 8 hadi 10.

Aidha RC Makonda ameipongeza Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa kazi kubwa na nzuri ya kutoa huduma za kisasa kwa wagonjwa jambo lililosaidia kuokoa gharama zilizokuwa zikitumika kusafirisha wagonjwa nje ya nchi.

Kwa upande wao wazazi wa watoto waliopata ufadhili huo kutoka mikoa mbalimbali wamemshukuru RC Makonda ambapo wameeleza kuwa kwa muda mrefu wamehangahika kutafuta pesa ya matibabu kwa watoto wao bila mafanikio kutokana na ukubwa wa garama.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad