Yanga Yafanya Maamuzi Magumu Kuhusu Ajibu

meelezwa kuwa uongozi wa Yanga umeamua kubadili gia angani kwa kuanza mazungumzo ya kumuogezea mkataba kiungo wao Ibrahim Ajibu ambaye mkataba wake umememalizika ndani ya Yanga.

Taarifa imeeleza kuwa kwa sasa Ajibu yupo kwenye mazungumzo na Yanga ili kuona namna gani atarejea ambapo viongozi wamekuja na gia mbadala kwa kuifuata familia ya Ajibu.

Taarifa zimeeleza kwamba baada ya kuona Ajibu amegomea ofa ya ktua TP Mazembe uongozi wa Yanga ukazungumza na familia ya Ajibu ambao wao wanapenda kuona kijana wao akiwa Jangwani huku habar zikieleza tayari amelamba mkataba kwenye timu yake ya zamani Simba.

Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredirick Mwakalebela amesema kuwa wanajua uwezo wa Ajibu ila kwa sasa suala la mkataba wake hawawezi kulizungumzia.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad