Ajali ya Ethiopia Airlines: Mwathiriwa akataa fidia kutoka Boeing


Mwanamume mmoja aliyepoteza familia yake ya watu watano katika ajali ya ndege ya Boeing ilioanguka nchini Ethiopia anasema kuwa yeye na familia za waathiriwa wengine wa mkasa huo hawatakubali fidia inayotolewa na kampuni hiyo ya ndege.

Boeing inasema kuwa itatoa $100m kwa miaka kadhaa kwa serikali za mtaa na mashirika yasio ya kiserikali kuzisaidia familia na jamii zilizoathirika na ajali hiyo ya ndege aina ya 737 MAX nchini Indonesia na Ethiopia.

Malipo hayo yatakayotolewa kwa miaka kadhaa hayatokani na kesi iliowasilishwa mahakamani baada ya ajali hiyo ambayo ilisababisha vifo vya takriban watu 346.

''Fedha hizo zinalenga kusaidia elimu na maisha ya familia na mipango ya jamii'', ilisema Boeing.


Lakini John Quindos Karanja aliyepoteza vizazi vitatu vya familia yake ambayo iliabiri ndege hiyo ya Ethiopia Airlines ikielekea nchini Kenya alipinga wazo hilo.

Anasema kwamba familia zote zilizopo Kenya na Ethiopia zina kundi moja la WhatsApp ambalo waliliidhinisha siku chache baada ya ajali hiyo.

Karanja anasema kwamba familia hizo hazijapata mawasiliano yoyote rasmi kutoka kwa Boeing na ziligundua habari hizo kutoka kwa vyombo vya habari.

Anasema kwamba familia zote zimechukua msimamo wa kutoshawishiwa na pendekezo lolote ambalo halijatolewa na mahakama ya haki.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad