AZAM Fc Mzigoni Leo Kagame Kumenyana na KCCA

AZAM Fc Mzigoni Leo Kagame Kumenyana na KCCA
MABINGWA watetezi Azam FC leo watakuwa kazini kumenyana na KCCA kwenye michuano ya Kagame inayoendelea nchini Rwanda.

Mchezo wa kwanza Azam FC walipata ushindi wa bao 1-0 mbele ya wapinzani wao Mukura FC bao lililopachikwa kimiani na Idd Seleman.

Kocha wa Azam FC, Ettiene Ndayiragije amesema kuwa wanatambua ugumu wa mashindano kutokana na kikosi chake kushindwa kuwa na spidi kali.

"Mashindano sio mepesi tatizo la kwenye mchezo wa kwanza ilikuwa ni spidi ila nimefanyia kazi na tutapambana kupatamatokeo chanya," amesema.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad