Dkt. Bashiru Yaonya Ndani ya CCM, ‘Wakupuuza Tu’

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Dkt. Bashiru Ally, ametoa wito kwa wanachama wa chama hicho kuwapuuza wale watu wanaoendeleza mjadala usiokuwa na tija ndani ya chama hicho, na akawahakikishia kwamba chama hicho kiko imara.

Dk. Bashiru  ameyasema hayo wakati akitoa pongezi kwa hatua ya wanaCCM Mkoa wa Dodoma, kutaka Kanali Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba, makatibu wastaafu wa CCM kuchukuliwa hatua.

Makatibu hao wastaafu wiki iliyopita, walimwandikia barua Pius Msekwa, Katibu wa Baraza la Viongozi Wastaafu wa CCM wakilalamikia kuchafuliwa na Cyprian Musiba, anayejitambulisha kuwa mtetezi wa Rais John Magufuli.

Kwenye barua hiyo, Makamba na Kinana wamelalamika kuchafuliwa na kuzushiwa huku wakidai serikali imeshindwa kuchukua hatua na kuhoji ulinzi ulinzi anaopewa mtu huyo anayewachafua.

“Wapuuzeni, hatuogopi kukosolewa, lakini hatuko tayari kudharauliwa, kutukanwa na kubezwa na majina yaliyo na kebehi na watu wasio na shukrani, hatujafunzwa hivyo, hatujazoea hivyo,” amesema Dkt. Bashiru

Aidha, amesema kuwa uongozi wa CCM hautaruhusu malumbano ndani ya chama hicho, huku akieleza kwamba mwenyekiti wake, Dkt. Magufuli yuko tayari kuwasamehe, ili kukijenga chama.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad