JPM Aagiza Familia ya Mujungi ijengewe Nyumba ya Kisasa


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemuagiza meneja wa wakala wa barabara mkoa wa Kagera kuijengea nyumba ya hadhi familia ya Leopord Mujungi aliyekuwa mkurugenzi wa barabara nchini na ambaye alisimamia Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha rami kutoka Dar es salaam hadi Mpaka wa Mtukula wilayani Misenyi mkoani Kagera ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake kwa kulitumikia taifa.

Rais Magufuli amesema hayo mara baada ya kufika nyumbani kwa marehemu Mujungi aliyefariki kwa kujipiga risasi miaka kadhaa iliyopita na kuagiza familia hiyo ijengewe nyumba ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake kwa kulitumikia taifa.

”Natambua mchango mkubwa wa mzee Mjungi alikuwa mkweli na alikuwa mwaminifu, mnaweza kuona mtu aliyekuwa mkurugenzi wa barabara zote hata nyumba yake ni ya kawaida, nakuagiza meneja wa Tanrods wasiliana na wizara nyumba ijengwe hapa hata kama ni shilingi milioni 50-100 ijengwe hapa” Ameagiza Rais Magufuli.

Akiwa njiani, Rais Magufuli amezungumza na wananchi katika eneo la Kyaka wilayani Missenyi, Kemondo wilayani Bukoba na Muleba ambapo akiwa wilayani Muleba amemuagiza pia waziri wa Nishati Dkt. Medadi Kaleman kwenda mkoani Kagera kutatua changamoto ya umeme, kufuatia kuwepo kwa wananchi ambao wamelipia umeme wa Rea awamu ya pili na hawajaunganishiwa umeme.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad