Kanye West Amuomba Msamaha Jay Z

Mashabiki wa muziki wa Kanye west wamehoji kwanini amemuomba msamaha rapa mwenzake Jay Z, kwenye ngoma yake mpya ya "brothers" ambayo amemshirikisha Charlie Wilson.

Mashabiki hao wamehoji baada ya kuisikiliza na kusoma maandishi yaliyopo katika ngoma hiyo , ambayo yalikuwa yanamlenga rapa Jay Z.

Maandishi ya ngoma hiyo yanasomeka kama, "nisamehe kwa kukupoteza , nakubali kwamba nimekukumbuka ,nimekukumbuka kwenye ile familia yetu na undugu wetu, nimekumbuka kusafiri na ndege na wewe kwenda jijini Paris na kukumbatiana , na kupokea simu yako ukinipigia".

Kanye west na Jay Z wameshafanya kazi pamoja kupitia album ya "Watch The Throne" ya mwaka 2011 na kutoa ngoma kali kama Otis, n**s in paris , No church in the wild na Welcome to the jungle.

Wawili hao kwasasa hawana ukaribu kama ule wa mwanzo , na hawajaonekana wakiwa pamoja kwa muda mrefu hivi sasa.



Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad