Kocha wa Yanga Aanza na Stamina Morogoro

Tundaman atoa sababu ya ugomvi wake na Matonya ALHAMISI , 11TH JUL , 2019 NA MWANDISHI WETU   Kapteni wa muziki wa Bongo Fleva Tundaman, amefunguka sababu za yeye kutokuwa na maelewano na msanii mwenzake Seif Shabani, maarufu kama Matonya.    Tundaman  Tundaman amesema hayo leo kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, na ameeleza chanzo cha wawili hao kuwa na tofauti ni Matonya kumuiga sauti yake.  "Wakati nakutana na Matonya alikuwa na ngoma mbili tu, baada ya kukutana na mimi ndio nikampa madini ya tone ya sauti yangu, yeye ndio ananiiga mimi sauti. Nakumbuka kipindi kile alikuwa anakaa Kariakoo akawa mshikaji wangu sana, tulitaka kuanzisha kundi na nilimmezesha ngoma nyingi na nilimuandikia ngoma, ana material yangu mengi".  Aidha Tundaman amesema hajawahi kusikiliza nyimbo za Dogo Janja, na jana ndio ilikua mara ya kwanza kusikiliza baada ya kiugundua kuwa wametumia neno moja la "Kibada" kwenye ngoma zao.
KATIKA kuhakikisha kikosi cha Yanga kinakuwa imara zaidi msimu ujao, Kocha Msaidizi wa timu hiyo, Noel Mwandila amewaanzisha tizi la kibabe wachezaji hao kwa kuanza na mazoezi ya kujenga stamina ili kuweza kuwa imara.

Kikosi cha Yanga kipo mkoani Morogoro ambako kimeweka kambi ya muda mrefu kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 23.

Yanga imeweka kambi Morogoro bila ya kocha mkuu Mwinyi Zahera ambaye yupo nyumbani kwake nchini Ufaransa baada ya kutolewa katika michuano ya Afcon ambapo anatarajia kuwasili baada ya muda mchache kumaliza mapumziko.

 Akizungumza na Championi Ijumaa, Mratibu wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kuwa, Kocha Mwandila ameanza na mazoezi ya stamina ya kukijenga kikosi kabla ya kuanza mazoezi magumu ili kuhakikisha anawaweka
wachezaji sawa.

“Mazoezi anayoyatoa kocha kwa sasa ni yale ya stamina ya kujenga wachezaji kama inavyojulikana mazoezi ya mwanzoni mwa msimu, wachezaji wanafanya mazoezi asubuhi na jioni huku mwalimu akiwa anaendelea kukipanga kikosi ili kiweze kuwa imara.

“Baada ya kumaliza mazoezi hayo, ndio kocha atakapoendelea na mazoezi mengine kwa ajili ya kukiimarisha kikosi ambapo mwalimu akifika ataendelea pale atakapopakuta,” alisema Hafidh
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad