Mwakyembe Atoa Onyo Kwa Wanaosambaza Picha za Ajali Mitandaoni

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amewaonya watu wanaopiga picha kwa simu mara tu zinapotokea ajali na kusambaza mitandaoni.

Mwakyembe ametoa onyo hilo leo Jumanne Julai 9, wakati wa shughuli ya kuaga miili ya wafanyakazi wa Azam Media waliofariki jana Julai 8, katika ajali ya gari kati ya Shelui na Igunga na kuongeza kuwa Sheria ya Makosa ya Mitandao inazuia kufanya hivyo.

"Niwaombe Watanzania tuendeleze utamaduni wa utu ndugu zetu wanapopata ajali, niwaombeni acheni tabia ya kupiga picha na kurusha kwenye mitandao, sheria ya mitandao inakataza, hatutazungumza tena hili ni onyo la mwisho" - Waziri Mwakyembe

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad