Mwanamume Aliyemshika Mvulana Nyeti Zake Afutiwa Mashtaka

Mwanamume wa miaka 79 raia wa China alifikishwa mbele ya mahakama moja nchini New Zealand kwa kumshika sehemu za siri za mtoto wa kiume katika chumba cha kubadilisha nguo baada ya kuogelea.

Lakini mtu huyo aliponea shtaka la unyanyasaji wa kingono licha ya kukiri kuwa alifanya kitendo hicho .

Jaji alikubaliana na hoja ya mshukiwa kuwa tabia hiyo ni sehemu ya utamaduni wa Wachina unaosharia upendo, vyombo vya habari vimeripoti.

Mahujaji wa DRC wanyimwa viza na Saudi Arabia
Watu wenye jinsia mbili ni wangapi Kenya?
Uhusiano wa Trump na Boris utakuwa wa ''kusisimua''
Kuna ukweli wowote katika 'utamaduni' huo na China inalizingumzia vipi suala hili?

Kilichotokea wakati wa kisa hicho?

Mwaka jana mwezi Agosti katika kituo cha kujiburudisha mjini Christchurch, mwanamume wa Kichina anayefahamika kama Ren Changfu alimuona mtoto mvulana akibadilisha nguo zake baada ya kuogelea na bila kufahamu kuwa mtoto huyo alkuwa na baba yake, Ren alimsogelea na kuanza kusema na nae huku akishika na kuchezae uume wa mtoto huyo huku akicheka na kuzishika tena, Vyombo vya habari vya New Zealand viliripoti.

Baba yake mtoto huyo alimuomba aachane nae la sivyo atapiga simu polisi na kumripoti kw autovu wa nidhamu.

Mwanamume huyo ambaye alihamia New Zealand mwaka 2009, aliwambia maafisa waliokuja kumkamata kuwa hakujua kitendo chake ni makosa na kuongeza kuwa mtoto huyo alimkumbusha mjukuu wake aliyepo China ambaye anampenda sana.

Binti ya Ren alitayarisha ripoti iliyosema kuwa nchini China kumshika mtoto wa kiume sehemu zake za siri na kuzichezea ni ishara ya kuonesha upendo.

Kwa nini watoto hawa kiislamu wametenganishwa na familia zao?
Jaji wa mahakama ya wilaya ya Christchurch, Alistair Garland alikubaliana na utetezi wake na kuamua kuwa Ren hakua na nia ya kumdhulumu kimapenzi mtoto huyo.

Aidha jaji alisema kuwa Ren ameshutuka sana kujua kuwa aliwakwaza vibaya wazazi wa mvulana huyo na kwamba "yuko tayari kufanya lolote ili asamehewe", na kuongeza kuw kosa hilo linastahili kueleweka kwa misingi ya utamaduni wajamii ya Bw. Ren".

Wazazi wa mtoto huyo wamekubali kumsamehe na pamoja na dola 670 alizolipa kufidia kosa lake.

Wachina wenyewe waanasema nini?

Kisa hicho kilizua mjadala mkali katika mitandao ya kijamii kote nchini China kwa zaidi ya wiki moja,baadhi ya watu wakisema kuwa alitafsiri vibaya utamaduni wa jamii yao.

Watu 300 kati ya 1200 waliojadili suala walihisi kuwa kitendo chake hakihusiani kwa vyovyote na utamnaduni wao.

Wengine karibu 200 walisema washawahi kusikia utamaduni kama huo lakini wanasema ni utamaduni uliopitwa na wakati japo bado unatumika miongoni mwa watu wanaoishi vijijini.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad