Ninja Alipwa Mshahara wa Bilioni 2 Marekani

Ninja Alipwa Mshahara wa Bilioni 2 Marekani
IMEFAHAMIKA kuwa beki wa zamani wa Yanga, Abdallah Shaibu ‘Ninja’ ambaye kwa sasa anakwenda LA Galaxy ya Marekani kwa mkopo, atakuwa akilipwa mshahara wa euro 18,000 (Sh milioni 46.7) kwa wiki, ambazo ni sawa na shilingi za Kitanzania bilioni 2.2 kwa mwaka.

Ninja ambaye amesaini mkataba wa miaka minne katika Klabu ya MFK Vyškov ya Jamhuri ya Czech, anapelekwa Marekani kucheza kwa mkopo wa mwaka mmoja.

Ninja aliyeitumikia Yanga kwa misimu miwili mfululizo akitokea katika Klabu ya Taifa Jang’ombe ya Zanzibar, ameamua kutafuta changamoto mpya nje ya nchi, baada ya mkataba wake na klabu hiyo kumalizika mwishoni mwa msimu huu huku akidaiwa kulamba mshahara wa zaidi ya euro elfu 18 kwa wiki ambayo ni zaidi ya Sh milioni 46.7 za Kitanzania.

Chanzo makini cha habari hii kimelinyetishia Championi Jumatano kuwa, Kampuni ya Dream World Sport, imemwezesha kuingia mkataba huo, ambao utamfanya
kulipwa kwa kila wiki kiasi hicho.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad