Rais Magufuli Ateua Mkuu wa Wilaya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Edward Mpogolo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida.

Uteuzi huu unaanza leo tarehe 24 Julai, 2019, Mpogolo anachukua nafasi ya Bw. Miraji Mtaturu ambaye amechaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Mpogolo alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma, nafasi ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma itajazwa baadaye.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad