Rais Magufuli kuwa mgeni rasmi maonyesho ya Nanenane

Rais John Magufuli anatarajia kuwa mgeni rasmi siku ya kilele cha Maonesho na Maadhimisho ya Nanenane kwa mwaka huu yanaotarajia kufanyika Nyakabindi Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.

Hayo yamesemwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka, wakati akizungumza na waandishi habari kuhusu maonesho hayo ya Nanenane yanatarajia kuanza 1/8/2019 hadi 8/9/2019.

RC Mtaka amesema katika maonesho hayo yanatafunguliwa na Makamu Samia Suluhu na  kauli mbiu yake ni Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa ukuaji wa uchumi kwa wananchi na yanatarajia kuwashirikisha watu mbali mbali na yana lengo la kuwainua wakulima, viwanda na wajasiliamiali mbalimbali.

RC Mtaka amesema katika maonesho hayo wanatarajia kuwashirikisha watu zaidi ya elfu 50 ambapo pia yatawashirikisha maofisa mbalimbali wa Serikali ambao watakuwa na shughuli za kuwasaidia wananchi huku akiwataka wakulima na wajasiriamali kujitokeza kwa wingi katika maonesho haya.

Kwa upande wake Kaimu Afisa Mtendaji wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni(BRELA) Emmanuel Kakwezi, amesema  katika maonesho hayo BRELA  watatoa huduma.

Kakwezi amewataka wananchi kujitokeza ili waweze kusajili biashara zao kwa urahisi katika msimu huu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad