Tetesi za SOKA Dirisha la Usajili Ulaya



Manchester United wanajianda kuweka dau la kumnunua kiungo wa safu ya kati wa Newcastle Muingereza Sean Longstaff, 21. (Sky Sports)

Manchester United na Paris St-Germain zimekubaliana malipo ya kumnunua mlinzi wa Ajax na Uholanzi Matthijs de Ligt, 19. (European football expert Julien Laurens, via Express)

Winga wa Chelsea na England Callum Hudson-Odoi, 18, anakaribia kutia saini mkataba mpya na klabu hiyo, Stamford Bridge. (Goal)

Arsenal huenda ikamsaini winga wa Uhispania Lucas Vazquez, 28, kwa mkataba wa pauni milioni 31 kutoka Real Madrid wiki ijayo. (AS)

Leicester inaelekea kuvunja rekodi ya uhamisho wa wachezaji kumsajili kiungo wa kati wa Monaco na Ubelgiji Belgium Youri Tielemans,22, ambaye aliyecheza kwa mkopo, uwanja wa King Power karibu nusu ya msimu uliyopita. (Leicester Mercury)

Tottenham inakaribia kukamilisha mpango wa kumsajili kiungo wa kati wa Real Madrid na Uhispania Dani Ceballos, 22. (AS)


Mshambuliaji wa Bournemouth na England Callum Wilson, 27, ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa West Ham msimu ujao. (90Min)

Hammers wamewasilisha ombi la kutaka kumnunua mshambulizi wa Celta Vigo na Uruguay Maxi Gomez,24, ambaye pia ananyatiwa na Valencia.(Evening Standard)

Liverpool pia wako tayari kumsaji Ceballos baada ya kutathmini kwa kina mpangao wao. (Sportwitness)


Spurs wanamtaka kiungo wa kati wa Roma na Italia Nicolo Zaniolo, 20. (Sportslens)

Kipa wa Newcastle United, Muingereza Karl Darlow, 28, analengwa na Blackburn Rovers. (Sky Sports)

Kocha wa zamani wa Manchester United na Chelsea Jose Mourinho amekataa ofa ya kuwa meneja wa klabu ya Guangzhou, ya China. (Guardian)



Mabingwa wa Uturuki Galatasaray wanataka kumsajili mshambuliaji wa Italia Stefano Okaka, 29. (Watford Observer)

Birmingham City wako tayari kupatia ofa ya majaribio mshambuliaji wa Stoke City, Saido Berahino,25. (Sun)



Tetesi Bora Ijumaa

Mchezaji Bruno Fernandes ameanza mchakato wa kuhamia Old Trafford. Nyota huyo wa miaka 24 anayecheza safu ya kati ya Sporting Lisbon na Ureno anatarajiwa kwenda Manchester kufanya vipimo vya afya. (Sport Witness)



Red Devils wanamlenga mlinzi wa Atletico Madrid na Uhispania Saul Niguez, 24, kuchukua nafasi ya Paul Pogba, endapo nyota huyo wa miaka 26 raia wa Ufaransa ataondoka Old Trafford. (Express)

Leicester wataelekeza nguvu zao zote kumsaini beki wa Burnley James Tarkowski endapo Harry Maguire ataenda klabu ya Man United.



Hata hivyo, Leicester wataminyana na Wolves katika harakati za kutaka kumsajili Tarkowski. (Birmingham City)

Arsenal watamkosa kipa wa Ujerumani wa miaka 21 Markus Schubert, ambaye ameamua kujiunga na Schalke kutoka Dynamo Dresden. (Sport1)

Arsenal pia wako mbioni kumsajili Marcelo baada ya beki huyo Mbrazil kuomba kuondoka Real Madrid. (Sport – via Metro)

Tetesi Bora Alhamisi

Gunners wana pauni milioni 70 wanapojianda kuweka dau la pili la kumnunua Zaha, japo kuwa Palace wanamini thamani ya mshambuliji huyo ni pauni milioni 80(Sky Sports)

Arsenal wamepewa nafasi ya kumsaini mshambuliaji wa Barcelona Mbrazil Malcom, 22, lakini azma yao kubwa ni kumnasa mshambuliaji wa Ivory Cost wa miaka 26, Wilfred Zaha kutoka Crystal Palace. (Mirror)

Frank Lampard amepigwa picha katika uwanja wa Stamford Bridge alipokaribia kuwa kocha mpya wa Chelsea. (Mail)

Chelsea pia imeanza mazungumzo ya kandarasi mpya ya na kiungo wa kati wa miaka 20 Mason Mount, ambaye aliichezea Derby msimu uliopita chini ya ukufunzi wa Lampard. (Evening Standard)

Tottenham imesitisha mazungumzo yake na Real Betis kumhusu kiungo ya kati wa Argentina Giovani Lo Celso, 24, baada ya vilabu kushindwa kuafikiana malipo. (Sky Sports)

Manchester United wanataka kumsajili mchezaji wa safu ya kati wa Ureno Bruno Fernandes, 24 kutoka Sporting Lisbon. (Sky Sports)
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad