Uingereza Yapata Waziri Mkuu Mpya

Waziri wa zamani wa mambo ya kigeni wa Uingereza Boris Johnson amechaguliwa kuwa kiongozi wa chama tawala cha Conservatives nchini humo atakayechukua mara moja nafasi ya Bi Theresa May.

Hii inamaanisha Boris Johnson sasa atakuwa Waziri Mkuu mpya wa Uingereza baada ya May kutangaza kujiuzulu mwezi uliyopita.

Boris aliye na miaka 55 alimshinda mpinzani wake Jeremy Hunt kwa wingi wa kura katika uchaguzi wa wanachama wa chama cha conservatives hii leo.

Waziri huyo wa masuala ya kigeni wa zamani wa Uingereza ananatarajiwa kuchukua rasmi nafasi hiyo ya uwaziri Mkuu hapo kesho Jumatano (24.07.2019).

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad