Waziri Mpango Atoa Tahadhari Kwa Taasisi Za Kifedha Kuwa Makini Na Mitandao Ya Kimataifa Ya Uhalifu.

Waziri wa Fedha na Mipango Dokta Philip Mpango amezitaka taasisi za kifedha hapa nchini kuwa makini na mitandao ya uhalifu ya  kimataifa.

Waziri Mpango amesema hayo leo Julai 8,2019  katika hafla fupi  ya kupokea  hundi ya gawio kwa  serikali kutoka benki ya NMB ambapo jumla ya Tsh.Bilioni 10.48 zimetolewa na Benki  hiyo kama gawio kwa serikali ambayo ni sehemu ya faida.

Waziri mpango amesema pamoja na mafanikio ya benki Ya huduma za kibenki hapa nchini lakini bado kuna changamoto za uhalifu wa kimtandao ambapo Wizara yake imepokea  kesi na malalamiko mbalimbali yanayotokana na uhalifu  wa  mitandao.

Hivyo Dokta Mpango ametoa tahadhari  kwa taasisi za kifedha  nchini  kuwa macho  na wahalifu na watakatishaji wa fedha   kupitia Mitandao ya kimataifa.

Mwenyekiti wa bodi ya Benki ya NMB Prof.Joseph Semboje amesema kwa kipindi cha miaka  10 iliyopita Benki hiyo ilishalipa Tsh.Milioni 118 serikalini kama gawio.

Naye Afisa mkuu wa Fedha kutoka benki ya NMB Bi.Ruth Saikuna amesema benki hiyo ilitengeneza faida ya Tsh.Bilioni 142 kwa  mwaka 2018 sawa na ongezeko la asilimia 3%.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad