Atakayenioa Hajulikani Kirahisi - Lulu Diva

MWANAMUZIKI anayefanya vizuri kwenye anga la Bongo Fleva, Lulu Abbas ‘Lulu Diva’ amefunguka kuwa licha ya watu kumhusisha na wanaume wengi tofauti lakini mwanaume halisi ambaye atamuoa hawatamjua kirahisi.  Akizungumza na Gazeti la Amani, Lulu Diva amesema mbali na wanaume wengi ambao watu wameona mapichapicha mitandaoni, mhusika halisi hawatamjua mpaka aamue.

“Unajua watu wanaona tu mitandaoni watashangazwa sana na mimi kwa sababu mengi yanayosemwa si ya kweli lakini siku watasikia tu nishaingia kwenye ndoa na ni mke wa mtu, mume wangu hawawezi kumjua kirahisi,” alisema Lulu Diva.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad