Aunt Ezekiel Naye Ajiongeza Afuata nyayo za Shilole, Irene Uwoya na Wema Sepetu

Staa wa filamu nchini, Aunt Ezekiel  aungana na mastaa mwenzake bongo, kujikita katika suala zima la ujasiriamali baada ya kufungua pub yake kubwa ya kisasa iliyopo Mikocheni, jijini Dar.

Aunt amefungua pub hiyo ya kisasa aliyoipa jina ya The Luxe.

The luxe ina sehemu kubwa ya kupumzikia kwa ndani na nje wakati ukipata vinywaji. Kama hiyo haitoshi, kwenye pub hiyo pia kuna sehemu ya chakula yenye mandhari tofauti ambayo inaweza kumvutia mteja kulingana na matakwa yake.

Kwa sasa mastaa wakike Bongo wanaonekana kujikita kwenye ujasiriamali zaidi ambapo mbali na Aunt na Uwoya kumiliki pub, wapo Zuwena Mohamed Shilole anayemiliki mgahawa na Wema Sepetu (duka la nguo).

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad