Dkt. Slaa acharuka, ‘Wanatupa shida sana ubalozini’


Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Dkt. Wilbord Slaa amekemea tabia ya baadhi ya Watanzania kubeza miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano huku akibainisha kuwa vitendo vya kutumia mitandao ya kijamii kukosoa utendaji wa serikali unawapa shida mabalozi kuitetea nchi huko walipo,kwasababu vitendo hivyo vinawakatisha tamaa wahisani wanaotaka kuisaidia Tanzania.

Ameyasema hayo wakati akifanya mahojiano na kituo cha televisheni cha Startv wakati wa ziara ya mabalozi wa Tanzania kutoka nchi mbalimbali duniani walipokuwa wakitembelea mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR eneo la Soga Mkoani Pwani.

Ametoa mfano kutokana na kauli aliyoitoa kiongozi flani ambaye hakumtaja imesababisha watalii 100 kutoka Sweden kuahirisha safari ya kuja Tanzania kwa ajili ya kutalii.

Hata hivyo, Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali wapo katika ziara ya kutembelea na kujionea miradi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya awamu ya tano kwa fedha za ndani

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Tatizo lililopo awamu hii ya uongozi kila anayekosoa serikali anaonekana ni adui, hilo ndilo tatizo lililopo mheshimiwa balozi Dk Slaa, hakuna mtu anayepinga miradi ya maendeleo, kinachopigiwa kelele ni kukandamiza ule uhuru wa kutoa mawazo.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mdau, mwelekeo wa fikra zako na Akili ya ilivyo jipanga. ina waakini.

      Kama una macho.. Basi ummefumba
      Kama una masikio .Umejitia Uziwi
      Kama Una Akili basi Unahitajii matibabu MIREMBE. KARIBU SANA.

      Vya Dhahirihuwa havina Mjadala.

      Au nawewe Mdau ndio wale wa Dadii? na sasa vyuma VIMEKAZA..?

      Delete

Top Post Ad

Below Post Ad