Dogo Janja atambulisha mpenzi mpya


Msanii wa Hip Hop nchini, Dogo Janja amemuweka wazi mpenzi wake mpya baada ya muda mrefu kupita tangu alipoachana na aliyekuwa mke wake, muigizaji Irene Uwoya.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Dogo Janja ameweka picha akiwa na mpenzi wake huyo mpya siku ya jana kwenye sikukuu ya Eid El Hajj na kuandika, “kipande hiki EID tunaimaliza kwa style hii.. happy moments with my baby!! Kenya 254 wagwaan”.

Hii sio mara ya kwanza kwa Dogo Janja kumuonyesha mpenzi wake huyo katika mtandao wa kijamii wa Instagram, huwa anam-post mara kwa mara huku akiandika maandishi yanayoashiria wana mahusiano.

Huyu anaweza akawa mrithi wa aliyekuwa mke wake, Irene Uwoya ambaye waliachana mwaka jana baada ya kudumu kwa kipindi kifupi kwenye ndoa. Pia Dogo Janja aliwahi kusema yupo tayari kuoa tena mwanamke mwingine.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad