Irene Uwoya Awatolea Uvivu Mashabiki Wake Wanaomsema Kuhusu Bata Anazokula


Mwigizaji Irene Uwoya ameamua kuyatoa ya moyoni kwa wale ambao wamekuwa wakimuandama kuhusu kujenga nyumba yake binafsi hii ni baada ya yeye kuonekana kula bata na kuwa sehemu mbalimbali za kifahari.

Kupitia ukurasa wa instagram wa Irene Uwoya amefanunua juu ya hilo na kusema kuwa sio lazima watu wote wajenge ikitokea kila mtu akajenga hakuna mtu atapanga hata hivyo alienda mbali na kusema watu wenye private life huwa hawaongei na meneno mengi huzuka kutokana na watu kukosa vy akuonyesha.

“Vichoroko :Irene mbona hujengi…kila siku bataaa Haya maisha tuuu kuna kesho
Me :tukijenga wote nani atapanga?sio lazima wote tujenge …wengine tutakuwa maua kwa bustaniii na nyie pambeni tu dunia kwa kujenga sisi tutapaka rangi kwa bata.Vichoroko :sio kwamba hatuna pesa yakwenda hotel au kujionyesha ila tunapenda private life Me: wenye private life hawaongeagi Bali nyie hamna vya kuonyesha.😷”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad