KATAVI: Mwili wa mtoto wakutwa makaburini


Mwili wa mtoto anayefahamika kwa jina la Kelvin Stephano (12), umeokotwa katika makaburi yaliyopo mtaa wa Nsemulwa kwa Mkumbo, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi ukiwa umekwishaharibika.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Rashid Mohamed, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, ambapo amesema kutokana na mwili wa marehemu kuharibika vibaya, haikuweza kubainika moja kwa moja  chanzo cha kifo chake.

Kwa upande wake Stephano Robart Makofia, ambaye ni mzazi wa marehemu amesema, alipofika eneo la tukio alimtambua mtoto wake kwa mavazi aliyokuwa amevaa siku aliyotoweka nyumbani.

Wakizungumza na EATV baadhi ya majirani wameitupia lawama familia hiyo, kwa madai walikuwa hawamjali mtoto wao.

Aidha Kamanda wa Polisi ametoa Rai kwa wazazi mkoani Katavi kuwa makini na watoto wao ili kuepuka majanga kama hayo kuwakuta watoto.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad