Kimenuka..Mwanafunzi Amshtaki Rais Yoweri Museven Kwa Kum Block Asitembelee Akauti yake ya Twitter


Hillary Innocent Seguya Taylor anayesoma shahada ya uzamili katika Chuo Kikuu cha Harvard amefungua kesi hiyo akiwashtaki, Rais Yoweri Museveni, Msemaji wa Serikali, Ofwono Opondo na Mkuu wa Kitengo cha Siasa ndani ya Idara ya Polisi, Asan Kaingye

Kijana huyo amefungua shauri hilo kupitia kwa Wakili wake Male Mabirizi kwa sababu yeye hayupo nchini Uganda kwa sasa, akilalamika kuzuiwa kupata taarifa

Anasema kuwa alizuiwa kuzitembelea akaunti hizo tatu kuanzia Julai, 20, 30 na Agosti 8 na kitendo ambacho kimesababishia ashindwe kutoa maoni yake kuhusu taarifa mbalimbali za masuala ya kiserikali wanazowekwa kupitia akaunti zao

Kupitia kwa wakili wake amewasilisha ushahidi wa Tweets 27 ambazo Rais Museveni aliziweka akitoa taarifa kuhusu utendaji wa Serikali ambazo yeye hazikumfikia

Kesi hii imefunguliwa kupitia Mahakama Kuu ya Uganda iliyopo Jijini Kampala

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad