Korea Kaskazini Yaanza Tena Majaribio ya Makombora

Korea Kaskazini yaanza tena majaribio ya makombora
Korea Kaskazini imemeanya upya majaribio ya makombora yake. Kulingana na duru za Korea Kaskazini makombora mawili yamefyatuliwa kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.

Makombora hayo yameanguka katika pwani ya bahari mashariki mwa nchi hiyo. Katika taarifa Wizara ya mambo ya nje ya Korea Kaskazini imesema luteka za pamoja za kijeshi kati yake na Marekani zilianza hapo jana.

Taarifa hiyo imezidi kusema kuwa luteka hizo ni muhimu kwa Korea Kaskazini kwani ilihitajika kutengeneza, kufanya majaribio na kuweka silaha hizo kwa ajili ya ulinzi wa kitaifa.

Korea Kaskazini tayari ilifanya majaribio ya makombora mawili wiki moja iliyopita.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad