Madee Atupa Dongo kwa Nikki Wa Pili, Mwana FA

Nguli wa Bongo Fleva na shabiki mkubwa wa timu ya Arsenal hapa nchini Tanzania Madee, amewapiga kijembe wasanii wenzake na mashabiki wa timu ya Manchester United ambao ni Nikki wa Pili Mwana Fa na Ommy Dimpoz.


Akipiga stori na EATV & EA Radio Digital, Madee amesema kuwa katika bara la Ulaya hakuna timu iliyofanya usajili mzuri kama Arsenal na kwamba Man United haiwezi kufika popote kwa usajili mbovu walioufanya.

“Timu yangu ya Arsenal ipo vizuri kila mahali na wategemee mambo makubwa msimu huu kwa sababu ya usajili ambao tumeufanya, ukizungumzia Ulaya nzima Arsenal ndio imefanya vizuri kwenye usajili, watu wasubiri kazi tu”

"Man United Wamemsajili beki mbovu Harry Maguire tena kwa gharama kubwa na atapata tabu sana atakapokutana na Nicholaus Pepe wa timu ya Arsenal", ameongeza.

Kabla ya kuanza kwa ligi ya Uingereza, siku kadhaa zilizopita Madee na Mwana FA walitambiana katika mtandao wa kijamii wa Twitter ambapo mjadala ulianza baada ya Madee kuandiaka,

“Mwambieni mkaka alietoa kibao matata we endelea tu 'Mwana FA' jezi zao wataishia kuvaa sebleni mwaka huu. Ni mbayaaaa, uzi wetu hata harusi unafungia'

Pia Mwana FA akamjibu kwa kuandika “kwani jezi ndio zinacheza mpira?”
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad