Ujumbe wa Dr Mwigulu Nchemba Kwenda Kwa Zitto Kabwe 'Ushindi wa Magufuli 2020 Utakuwa wa Kishindo'


Bwana ZITTO, Elewa kuwa Rais Yuko kazini, Hajakutana na watendaji Kama mwenyekiti wa Chama. Hata angekutana kwa ajili ya UCHAGUZI kwa mtu mwenye akili timamu ungejua kuwa UCHAGUZI wowote huandaliwa na Serikali iliyoko MADARAKANI kwa kutumia watumishi wa UMMA.

1) CCM Ni Chama Cha Wakulima na Wafanyakazi wakiwepo watumishi, Hivyo watumishi wakikiunga mkono Chama na Chama kikawategemea sio dhambi. Vyama vingine havina kundi lolote la WATANZANIA vinategemea wakoloni.

2) Rais Hana haja ya kuwaelekeza Ma DSOs Na Ma RSOs kuiba kura kwa sababu kwa KAZI alizofanya kura tayari anazo, Shida yako ZITTO hata jimboni kwako hutembelei ujue kuwa kura anazo. Jimboni KWANGU Rais hata asipokuja kufanya Kampeni, Miradi ya maendeleo imeshampigia KAMPENI KURA ANAZO. HAYA MAMBO UNAYOTAKA KUIBA, KUELEKEZA, tunajua lengo Ni kuchafua na kuandaa visingizio.

USHINDI ITAKAOPATA CCM Serikali za Mitaa na USHINDI ATAKAOPATA RAIS MAGUFULI 2020 UTAKUWA WA KIHISTORIA AMBAO HAUJAWAHIPATIKANA. ITAKUWA CHAGUA MAGUFULI KAZI IENDELEEE.......
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad