Makubwa...Mtoto wa Mwaka Mmoja Anusurika Kufa Baada ya Kubwia Dawa za Kulevya..



Mtoto huyo (jina linahifadhiwa), alifikishwa Hospitali ya Mnazi Mmoja Agosti 18, mwaka huu kwa ajili ya matibabu baada ya kudaiwa kubwia #DawaZaKulevya aina ya ‘cocaine’

Katibu wa hospitali hiyo ya Mjini Magharibi, Hassan Makame amesema mtoto alipofikishwa hospitalini alikuwa analia sana hivyo alichomwa sindano ya usingizi na kuwekewa maji ya dripu

Ameongeza kuwa "Baada ya kupatiwa huduma hiyo mtoto huyo alilala na alipoamka alipata nafuu na alikaa hospitali kwa muda wa siku mbili na kutolewa hospitali Agosti 21"

Mama mzazi wa mtoto alieleza kuwa mtoto wake aliokota dawa hizo asubuhi siku hiyo na baada ya kula unga huo walimpa maziwa na kuanza kutapika

Baadaye hali ya mtoto ilibadilika na kumpeleka hospitali moja binafsi na kupatiwa huduma na waliporejea nyumbani hali yake haikuwa nzuri na ndipo alimpeleka Mnazi Mmoja

Aidha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Thobias Sedeyoka amesema Polisi inaendelea na uchunguzi na mama wa mtoto yupo chini ya uangalizi wa Polisi kwa ajili ya upelelezi

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad