Marekani Yazuia Mali Zote za Venezuela.

Marekani Yazuia Mali Zote za Venezuela.
Utawala wa Rais Donald Trump umezuia mali zote za serikali ya Venezuela zilizopo nchini Marekani.

Amri hiyo inazihusu mali zote za serikali ya Venezuela pamoja na zile zinazoweza kumilikiwa na mtu yoyote aliyeko nchini Marekani.

Utawala wa Trump pamoja na serikali kadhaa za nchi za Amerika ya Kati zinamtaka Rais Nicolas Maduro ajiuzulu ili kumwezesha kiongozi wa upinzani, Juan Guaido achukue madaraka.

 Amri ya Rais Trump imetolewa kutokana na kuendelea kwa mgogoro wa haki za binadamu nchini Venezuela.

Watu wa Venezuela zaidi ya milioni 4 wameshaondoka nchini humo kutokana na shida za kiuchumi na uhaba wa chakula.

Wakati huohuo Rais wa Colombia Ivan Duque ametangaza kuwa nchi yake itawapa uraia watoto 24,000 waliozaliwa na wazazi kutoka Venezuela kuanzia mwezi Agosti mwaka 2015.

Watu zaidi ya milioni 1.4 kutoka Venezueka walivuka mpaka na kuingia Colombia ili kuepuka athari za mgogoro na uhaba sugu wa mahitaji muhimu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad