Mastaa Bongo Wachomoza Tuzo za Afrima Nigeria




MSIMU wa sita wa tuzo kubwa za muziki Afrika zenye ushirikiano na Umoja wa Mataifa ya Afrika (AU), All Africa Music Awards (AFRIMA 2019), umewadia na majina ya wasanii wanaowania vipengele mbalimbali yametajwa.

Katika tuzo hizo zinazotarajiwa kutolewa Novemba mwaka huu, Tanzania imeendelea kufanya vizuri kwa kutoa wasanii Diamond Platnumz, Vanessa Mdee, Rayvanny, Harmonize, Maua Sama, Queen Darling, Rosa Ree, Nandy na Mbosso.

Akizungumzia tuzo hizo, Mbosso alisema: “Kuingia kwenye tuzo hizi ni jambo kubwa kwa sababu ni tuzo zenye heshima.”
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad