Mawakili wanne kumtetea Lissu, Kibatala ndani

Mawakili wanne wanatarajiwa kuanza kumtetea aliyekuwa mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu  aliyevuliwa wadhifa huo hivi karibuni.

Lissu yuko nchini Ubelgiji alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi na watu ambao hadi sasa hawajajulikana, alifungua rasmi shauri hilo jana.

 Alute Mughwai kaka yake Lissu akizungumza na waandishi wa habari  amesema kesi hiyo itaanza kuunguruma Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

Mawakili hao wataongozwa na Kibatala na wengine ni Jeremia Mbesya, John Malya na Fredi Kalonga.

Amebainisha kuwa maombi ya kufunguliwa kesi hiyo  chini ya hati ya dharura, kupitia kwake (Mughwai) aliyempa mamlaka ya kisheria kufanya hivyo, yatasikilizwa Agosti 21, 2019.

Mughwai  amesema wanatarajia Lissu kurejea Tanzania Septemba 7, 2019 baada ya uchunguzi wa mwisho wa madaktari wake utakaofanyika Agosti 20, 2019.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ndugu wanahabari wenzangu. Kwa heshima naweledi wa kazi zetu.
    Huyu mssaliti aliye ipaka Matope na anaendelea hivyo anacho taka kwa sasa ni kuwa Mitandaoni na Magazetini.
    Naomba Tumchunie..!!!

    Kama ni kesi basi watanzaania wengi wanazo na wala hatuzisikii wala kuziona na yake kama itatupiiwa mbali
    au kusikilizwa na kufungwa manake ni kwa maombia ya hati ya Dharura. Ambayo kila Mtanzania ana haki nayo na nyigi hufungwa naa kutupiliwambali baada ya kukosa mashiko na mapungufu ya kisheria katika Uwasilishaji.

    Naomba kwetu sisi tuwe na weledi na kujua tunacho taka kuandika kwa uelewa japo mdogo kama inabidi kuandika.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mdau uko sahihi,
      Aatakakula hela za Dezo za Walipa kodi.
      Ndugai ameamua kwa Wabunge Hewa kuzkiatia na kuziba Hewa.
      nchi iikwa pabaya..!
      ₩afanyakazi Hewa
      Wanafunzi Hewa
      Pembejeo Hewa
      Kaya maskini Hewa
      Mikoppo Hewa

      Wabunge Hewa (Lissu umeshtukiwa)

      Delete

Top Post Ad

Below Post Ad