Mbaroni Wakiuza Juice ya Nguvu za Kiume

Mbaroni Wakiuza Juice ya Nguvu za Kiume
Mamlaka ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar (ZFDA), imewakamata watu wawili kwa tuhuma za kuuza juisi ya tende iliyochanganywa na dawa ya kuongeza nguvu za kiume, kitendo kilichoelezwa kuwa si cha kibinadamu kwani dawa hizo huwa zinatolewa kwa utaratibu maalumu.


Hayo yamebainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa ZFDA Nassir Buheti, ambapo ameyataja maeneo ambayo juice hiyo ilikuwa ikiuzwa kuwa ni Fuoni, Kiembesamaki, Mwanakwerekwe na Magari ya Mawe, na kuwataja watuhumiwa hao kuwa ni Hamid Salum na Hemed Salum, ambao wamekuwa wakiuza juice hiyo kwa watu mbalimbali.

"Walichofanya ni jambo la hatari kwa afya ya binadamu, lengo lao ni kuwavutia watu kuongeza nguvu za kiume, kumbe wanachanganya na dawa hizi wanaziita '4G kifurushi cha wiki', pia hawana kibali kwa upande wa chakula. Na aina ya dawa wanazoziuza zinatakiwa kutolewa kwa cheti maalumu," amesema Buheti.

Kwa upande wa watuhumiwa hao wamekiri kuchanganya juice ya tende na dawa ya kuongeza nguvu za kiume aina ya 4G - Viagra, ambayo walikuwa wakizinunua kwenye maduka ya dawa kwa lengo la kuwavutia wanaume na walikuwa wakisambaza juice hiyo kwa kutumia gari aina ya Spacio.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad