Mchungaji TD Jakes kutoka Marekani Azua Gumzo Kenya, kupata nae Chakula Inakugharimu zaidi ya Mil 1.7 za Kitanzania



Gharama za kupata chakula cha usiku na askofu wa marekani TD Jakes zawa gumzo Kenya. Askofu huyo ambaye jina lake halisi ni Thomas Dexter Jakes atakua katika mkutano mkuu wa viongozi na wafanyabiashara utakaofanyika eneo la Kasarani jijini Nairobi mwezi ujao.


Ili kuingia eneo hilo utapaswa kulipia kiasi cha Dola 750 za kimarekani sawa na elfu sabini na tano za kenya ili tu waweze kuwa eneo moja na Askofu huyo.


Hata hivyo limeibuka gumzo mtandaoni kuhusu watu kulipa pesa ili kupata mlo na mchungaji huyo mwenye umaarufu mkubwa duniani. “Mchungaji abaki kuwa mchungaji jamani”, pesa yote hiyo kulikoni? moja ya maoni mtandaoni.

Chanzo BBC.

By Ally Juma.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad